Monday, July 31, 2017

WANANCHI MONDULI KUNUFAIKA NA MAJI



Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim (kushoto) na Andrew Chung ambaye ni mbunifu wa mtambo wa kusafisha maji wakionyesha mtambo huo kwenye uzinduzi wake kwenye kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha
Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim (kushoto) na mchungaji wa kanisa la Enyora Daniel Vengei wakiwa kwenye uzinduzi wake katika kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha.
Wananchi wa kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha wakishuhudia uzinduzi wa mtambo wa kusafisha maji na kuyachuja uliofanywa na kampuni ya Korea ya Smart Vision.

………………………….
Zaidi ya kaya 700 za wananchi wa Kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha, waliokuwa wanatumia maji ya kwenye bwana wanatarajia kunufaika na mradi wa kusafisha maji na kuchuja maji kuwa safi uliozinduliwa Kijiji hapo.

Awali, wananchi hao walikuwa wanatumia kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kupika, kufua, kuoga na kunywa maji hayo ya bwawa ambayo pia yalikuwa yanatumiwa na mifugo ya eneo hilo.

Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim akizungumza jana kwenye uzinduzi wa mradi alisema lengo ni jamii ya eneo hilo kunufaika na maji safi na salama yanayochujwa kupitia ubunifu wao.

Kim alisema kwa kuanza kuwanufaisha wananchi wa eneo hilo, wanatarajia kugawa majiko rafiki ya mazingira 22 na mitambo ya kuchuja na kusafisha maji ya bwawa kuwa safi na salama 22 kwa kaya 22 zitakazowanufaisha zaidi ya watu 220.

Alisema Smart Vision kupitia uwekezaji wa Korea Trade-Investment Promotion Agency. (KOTRA) jamii ya eneo hilo itanufaika na na mradi huo wenye lengo la kuondokana na matumizi ya maji yasiyo safi wala salama ambayo yanasababisha magonjwa ya tumbo.

“Jamii ya eneo hili kupitia mchungaji wa kanisa la Enyorata Daniel Vengei, walileta maombi kwetu kuwa wanatatizo la maji, hospitali na shule, ndipo tukaona tuanze kutatua hili suala la maji ndipo tukaleta mitambo hii ya kuchuja na kusafisha maji,” alisema Kim.

She said goal of project, Smart Vision head about maasai water problem in Korea. Smart Vision developed water purifier to help maasai people overcome water problem.

Kim said now Smart Vision a Korean Environmental company launches water project ina Tanzania, hopes to expand project to other parts of Tanzania where there is lack of drinking water.

“This project was aided financially bya KOTRA (Korea Trade-Investiment Promotion Agency) who supports international business of Korean companies, specifically, the KOTRA branc in Dar es salaam gave Smart Vision immense support in order to help people suffering from lack of drinking water though the water purification project,” said Kim.

She said people who helped with project is Director of Smart Vision Seo-Young Kim, Manager of Smart Vision, Hyun-Jung Chung and Purifier developer and volunteer, Andrew Chung.

Mkazi wa Kitongoji cha Emairete Rose Lemomo alisema alisema awali walikuwa wanakabiliwa na tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama lakini kupitia mradi huo wataondokana na maradhi ya tumbo yaliyokuwa yakiwakabili hasa watoto.

Lemomo aliwashukuru wote waliohusika na kufanikisha mradi huo, kwani hivi sasa watakuwa wanachota maji bwawani na kuyachuja na kuyasafisha kupitia mitambo hiyo.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Irmorijo, Mirishi Songoyo alishukuru shirika la Smart Vision kwa kufanikisha mradi huo wa maendeleo ambao utainufaisha jamii ya eneo hilo walioteseka kwa muda mrefu juu ya suala la maji.

“Tunawaomba wananchi watakaofikiwa na mradi huu kuhakikisha wanawasaidia na wale ambao bado wanasubiri kupatiwa majiko na mitambo ya kuchuja na kusafisha maji,” alisema Songoyo.

Mwalimu wa shule ya msingi Irmorijo, Stephen Laizer aliwataka wananchi wote waliofanikiwa kupatiwa mradi huo kuhakikisha wanautunza ili kunufaika nao kwa muda mrefu kwani wameteseka kwa miaka mingi kwenye tatizo la maji.

“Wageni wanapokuja kwenu inawabidi kuwashukuru hata kama hawajaacha chochote ila hawa wametuletea teknolojia ya maji, wanaweza kutufanyia mengine mazuri,” alisema Laizer.

No comments: