Tuesday, February 28, 2017

TNRF yazindua mpango mkakati wa Ardhi

Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo(aliyesimama) akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi hapa nchini Tanzania ambao utajumuisha mradi wa majaribio katika mikoa mbalimbali kuona kama utawezekana maana swala la upatikanaji wa ardhi imekuwa ni changamoto kubwa sana hapa nchini.
Mkurugenzi wa Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF), Joseph Olila akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi hapa nchini Tanzania uliodhaminiwa na Jumuiko la Maliasili Tanzania ili kuweza kupatikana kwa ardhi hasa maeneo ya vijijini .
Mkurugenzi Mtendani wa Taasisi ya MVUWATA ya Morogoro, Steven Ruvuga akizungumza jinsi wanavyoweza kuhamasisha watu kwenye matumizi mazuri yaardhi pamoja na kutatua migogoro ya ardhi kwenye mkutano uliofanyika kwneye ukumbi wa Hotel ya Wanyama jijini Dar es Salaam.
Bwana Alain Essimi  Biloa  akitoa mada juu ya matumizi mazuri ya ardhi kwenye jamii hasa kwa wananchi waishio vijijini
Baadhi ya wadau wakichangia mada kwenye kongamano lililofanyika leo katika Hotel ya Wanyama jijini Dar es Salaam leo
Baadhi ya wadau wakiwa kwenye mkutano wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi unaoratibiwa na Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF).
Meneja Program wa Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF), Zakaria Faustine akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi hapa nchini Tanzania ambao utajumuisha mradi wa majaribio katika mikoa mbalimbali 
Afisa Program za Ardhi Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF),Godfrey Massay akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkakati waliojiwekea kama Jumuiko la Maliasili Tanzania(TNRF) ili kufikia malengo  waliyojiwekea.
Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya kufanya uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi utakaoleta tija kwa wananchi hasa vijijini.
Picha ya Pamoja

No comments: