Wednesday, August 31, 2016

YALIYOJILI KATIKA MKUTANO WA PILI WA MWAKA WA NCHI 7 ZA AFRIKA MASHARIKI ZILIZO KATIKA MAPAMBANO YA KUTOKOMEZA TRAKOMA JIJINI ARUSHA


Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa ya Kupambana na Trakoma (ITI) akizungumza na washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma kuhusu uendelezaji wa juhudi za kuwaelimisha wananchi na kutoa tiba katika maeneo  yanakabiliwa na ugonjwa Trakoma kwa nchi washiriki wa mkutano huo kutoka Kenya, Tanzania, Uganda, Ethiopia, Eritrea, Sudani na Sudani Kusini.

Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Upendo John Mwingira akiwasilisha kuhusu mkakati wa kukabiliana na Trakoma kwa kuyafikia maeneo yasiyofikika kirahisi ya jamii za wafugaji nchini Tanzania wakati Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo  unaofanyika  jijini Arusha. Wananchi kutoka Jamii za wafugaji kutoka nchi washiriki wa mkutano huo bado wanakabiliwa na changamoto ya ugonjwa wa Trakoma.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Frida Mokiti akichangia wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.
Mshiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma Kutoka nchini Kenya Dkt. Rebecca Oenga akitoa uzoefu wa nchi ya Kenya katika kukabiliana na Trakoma  kwenye maeneo ya mipakani  ya jamii za wafugaji.
Afisa Afya kutoka Kaunti ya NAROK nchini Kenya Daniel Sironka akitoa mchango wake kuhusu namna anavyowaelimisha wananchi wa eneo lake kujikinga na kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la Sightsavers, Michael Kelly (katikati) akisisitiza jambo kuhusu ushiriki wa Sightsavers katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakati wa mkutano wa pili wa
mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.
Washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano huo jijini Arusha.
 Washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano huo jijini Arusha.


Washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma kutoka Tanzania wakiwa katika majadiliano kabla ya kuwasilisha taarifa ya pamoja kuhusu maeneo ya utekelezaji katika mapambano dhidi ya Trakoma.
Picha/Aron Msigwa –MAELEZO.

No comments: