Monday, February 29, 2016

WAKENYA WAENDELEA KUTAMBA KATIKA MBIO ZA KILIMANJARO MARATHONI 2016

Washiriki wa Mbio za Kilometa 42 katika mashindano ya kimataifa ya Kilimanjaro Marathoni 2016 wakianza mbio zao katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika Moshi (MOCU) .
Mshindi wa kwanza katika Mbio za Kilimanjaro  Marathoni Km 42 upande wa wanaume ,Kiprotich Kirui raia wa Kenya akihitimisha mbio katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika baada ya kutumia muda wa saa 2:16:43.
Mshiriki wa pili katika Mbio za Kilimanjaro Marathoni Km 42 upande wa wanaume ,Kenneth Ronoh raia wa Kenya akihitimisha mbio katika uwanja wa Chuo kikuu Cha Ushirika Moshi baada ya kutumia muda wa saa 2:16:48.
Mshindi wa kwanza katika Mbio za Kilimanjaro  Marathoni Km 42 upande wa wanawake Alice Kibor raia wa Kenya akihitimisha mbio huku akipiga ishara ya msalaba katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika baada ya kutumia muda wa saa 2:38:03.
 
Mshindi wa pili katika Mbio za Kilimanjaro  Marathoni Km 42 upande wa wanawake E Chemweno r raia wa Kenya akihitimisha mbio huku akipiga ishara ya msalaba katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika baada ya kutumia muda wa saa 2:44:20.

Mkurugenzi wa Masoko wa TBL Group Kushila Thomas akikabidhi bahasha ya zawadi kwa washindi wa Mbio za Kilimanjaro Marathoni 2016 upande wa wanawake.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo ,Nape Nnauye akisalimiana na mshindi wa pili katika mbio za Km 42 E,Chemweno kabla ya kumviha medali.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo ,Nape Nnauyeakikabidhi mfano wa hundi kwa washindi wa kwanza hadi wa tatu kwa wanawake katika mbio za Km 42.
Washindi wa kwanza hadi wa 10 wakiwa katika picha ya pamoja na  Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo ,Nape Nnauye.
 
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL Group Kushila Thomas akikabidhi bahasha ya zawadi kwa washindi wa Mbio za Kilimanjaro Marathoni 2016  km 42 upande wa wanaume.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo ,Nape Nnauyeakikabidhi mfano wa hundi kwa washindi wa kwanza hadi wa tatu kwa wanawake katika mbio za Km 42.
.Washindi wa kwanza hadi wa 10 wakiwa katika picha ya pamoja na  Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo ,Nape Nnauye. 
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL Group Kushila Thomas akitoa hotuba yake wakiwa ndio wadhamini wakuu wa Mbio za Kilimanjaro Marathoni 2016  
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania ,Anthony Mtaka akizungumza katika hitimisho la mashindano ya kimataifa ya mbio za Kilimanjaro Marathoni 2016.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: