Tuesday, June 30, 2015

TIMU YA WATU 21 YA KAMPUNI YA KUCHIMBA DHAHABU YA ACACIA WASHUKA KUTOKA MLIMA KILIMANJARO,WACHANGISHA MILIONI 800 KWA AJILI YA ELIMU TANZANIA.

Timu ya watu 21 ya wafanyakazi ,Ndugu na Marafiki wa Kampuni ya kuchimba dhahabu ya Acacia wakishuka kutoka mlima Kilimanjaro ambako walipanda kwa ajili ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia elimu.
Afisa Mtendaji mkuu wa Kampuni ya uchimbaji wa Dhahabu ya Acacia,Brad Gordon akiwa na Meneja wa Ustawi wa kampuni Asa Mwaipopo wakifurahia mara baada ya kushuka toka kaika kilele cha Uhuru ambako watu 19 kati ya 21 ndio walifanikiwa kufika kileleni.
Meneja wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa kampuni ya kuchimba Dhahabu ya Acacia,Necta P Foya akishangilia wakati akishuka toka mlima Kilimanjaro.
Timu ya watu 21 iliyopanda Mlima Kilimanjaro kutoka kampuni ya Kuchimba Dhabu ya Acacia wakiwa katika Uniform maalumu wakielekea lango la kutokea katika mlima la Mweka huku wakiimba nyimbo mbalimbali .
Mkuu wa wilaya ya Tarime ambaye alikuwa ni mgeni rasmi katika mapokezi ya timu ya watu 21 iliyopanda mlima Kilimanjaro,G;orious Luoga (wa tatu toka kushoto) akiimba na wapandaji hao.
Wapandaji wakiimba mara baada ya kufika katika lango la Mweka,hapa wakiongozwa nyimbo mbalimbali na mmoja wa asakari wa Hifadhi ya taifa ya Mlima Kiliamanjaro.
Afisa mtendaji mkuu wa Kampuni ya kuchimba Dhahabu ,Brad Gordon akifurahia na wafanyakazi wa kampuni hiyo,Meneja wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma,Necta Foya na Fredrick Njoka .
Timu ya watu 21 waliopanda mlima Kilimanjaro,wakiwa katika picha ya Pamoja katika lango la Mweka mara baada ya kushuka toka Kilele cha Uhuru.
Baadhi ya washiriki wa zoezi hilo la kupanda Mlima Kilimanjaro.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime ,Glorious Luoga akiteta jambo na Afisa Mtendaji mkuu wa kampuni ya kuchimba Dhahabu ya Acacia.
Makamu wa Rais wa Kampuni ya kuchimba Dhahabu ya Acacia,Deo Mwanyika akizungumza wakati wa hafla fupi ya mapokezi kwa timu iliyoshiriki kupanda Mlima Kilimanjro kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya shule za Msingi.
Mkuu wa wilaya ya Tarime,Glorious Luoga akizungumza katika hafla hiyo.
Afisa Mtendaji mkuu wa Kampuni ya Acacia ,Brad Gordon akikabidhi mfano wa hundi ya kiasi cha Shilingi Milioni 8,000,000 kwa mkuu wa wilaya ya Tarime ,Glorious Luoga ,zilizochangwa kupitia mpango wa CanEducate kwa ajili ya kusaidia elimu Tanzania.
Mkuu wa wilaya ya Tarime,Glorious Luoga akiwa amenyanyua juu  mfano wa Hundi.
Kaimu Mhifadhi Mkuu Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro,Charles Ngemba akizungumza wakati wa hafla fupi ya mapokezi ya timu ya watu 21 wakiwemo wafanyakazi ,Ndugu na marafiki wa kampuni ya kuchimba Dhahabu ya Acacia.

Na Dixon Busagaga wa Globu 

ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: