Tuesday, December 31, 2013

JAMAA APANDA JUU YA MNARA WA SIMU UBUNGO JIJINI DAR LEO NA KUGOMA KUSHUKA MPAKA AONANE NA RAISI KIKWETE

 Askari wa Kikosi cha Zima moto na Uokoaji Wakiwa wamepanda juu ya Mnara wa Simu Uliopo Ubungo Jijini Dar Es Salaam Muda mfupi uliopita kwaajili ya kumuokoa kijana mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Hassan Ambaye alipanda juu ya mnara huo kwa lengo la kufikisha Ujumbe wa kutaka kuonana na Raisi Kikwete ili aweze kumwelezea kwa kile anachodai kuwa jeshi la polisi lilimbambikia kesi na hatimaye kuhukumiwa kifungo cha Miaka 6 kwenda jela.

 Askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji wakiendelea na zoezi la kumuokoa Kijana Hassan kwaajili ya kutojirusha kutoka Juu ya Mnara wa Simu Muda mfupi uliopita Ubungo Jijini Dar Es Salaam Leo
Hapa akishushwa na askari wa Kikosi Cha Zimamoto na Uokoaji
Hapa Askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji akiwa amemuweka begani na Kushuka nae chini Mara baada ya kufanikiwa Kumshika vizuri kwaajili ya kumteremsha chini bila kupata madhara
 Kijana aliyefahamika kwa jina moja la Hassan akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kushushwa juu ya Mnara wa Simu na Askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji muda mfupi uliopita Ubungo jijini Dar
 Tukio likiendelea huku wakazi wa jiji la Dar Wakiendelea kushuhudia. 
 Raia wakishuhudia tukio hilo
 Wakazi wa Jiji la Dar wakishuhudia tukio hilo lililotokea muda mfupi uliopita Ubungo Jijini Dar leo
Gari la Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji likiwa limetia timu eneo la tukio kwaajili ya Kuokoa

Wakazi wa Jiji la Dar wakishuhudia gari la Polisi likiondoka na Kijana Hassan ambaye alipanda juu ya Mnara leo Ubungo jijini Dar Es Salaam.Picha Zote na Josephat Lukaza Wa Lukaza Blog

No comments: