Sunday, June 30, 2013

MAMA SALMA KIKWETE NA WAKE WA MARAIS WALIOKUWA KWENYE MKUTANO WA SMART PARTNERSHIP WATEMBELEA MAONESHO

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na waandishi wa habari mara tu baada ya kumaliza ziara yake na ugeni aliouongoza kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho tarehe 30.6.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifuatana na ,mke wa Mfalme Mswati wa Swaziland Inkhosikati Lambikiza (kushoto) na Waziri wa Jinsia, watoto na familia wa DR Congo ambaye amemwakilisha mke wa Rais Joseph Kabila Mheshimiwa Inagosi Bulo na mke wa Makamu wa Rais wa Zambia Mama Charlotte Scott wakianza kutembelea mabanda kwenye uwanja wa maonesho wa Mwalimu Nyerere, kwenye barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam tarehe 30.6.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiandamana na Mheshimiwa Inagosi Bulo kutoka DRC (kushoto) na Inkhosikati Lambikiza wa Swaziland na Mama Charlotte Scott wa Zambia wakiwa nje ya banda la Zanzibar mara baada ya kutembelea banda hilo.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Maendeleo Mama Salma Kikwete akiangalia bidhaa mbalimbali za aina ya shanga zilizokuwa zikionyeshwa kwenye banda la SIDO wakati walipotembelea maonesho hayo tarehe 30.6.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na wageni wake wakiangalia mashine ya kutengeneza nguo aina ya vikoi kwenye banda la SIDO wakati walipotembelea banda hilo tarehe 30.6.2013.
Mwenyekiti wa WAMA na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiagana na Mke wa Makamu wa Rais wa Zambia Mama Charlotte Scott ambaye aliondoka uwanjani hapo kwenda uwanja wa ndege kuungana na mume wake kwa ajili ya safari bya kurudi nchini Zambia.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifuatana na Waziri Inagosi Bulo kutoka DRC (kushoto) na Inkhosikati Lambikiza wa Swaziland (kulia) wakiangalia bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa kutoka kwenye mnazi kama zilivyokuwa zikionyeshwa na akina mama kwenye banda la WIPE.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifuatana na wageni wake wakitembelea mabanda mbalimbali ya maonesho wakiongozwa na Naibu wa Waziri wa Viwanda na Biashara Mheshimiwa Gregory Teu tarehe 30.6.2013.

No comments: