Tuesday, October 30, 2012

MAPATO UWANJA WA NDEGE PEMBA HAYAKIDHI MAHITAJI

Na Nafisa Madai 

Wafanyakazi wa kiwanja cha ndege Pemba wamesema mapatao yanayopatika kiwanjani hapo hayakidhi mahitaji ya kiwanja hivyo serikali kupitia wizara husika wanahitaji kutupia macho na nguvu zao kiwanjani hapo. 

Wamesema hayo wakati walipotembelea na waziri wa miundombinu na mawasiliano Mhe Rashid Seif ambapo wamesema kwa vile sasa wanatakiwa kubadilika kiutendaji tokea kuundwa kuwa mamlaka kamili serikali haina budi kuelekeza nguvu zao kiwanjani hapo ili kukifanya kiwanja hicho kuwa na hadhi na haiba nzuri kwa wenyeji na wageni wanaotumia kiwanja hicho. 

Aidha wamesema mpaka saivi bado hawajaona mabadiliko yoyote tokea kundwa mamlaka Jambo ambalo limekua likirudisha nyuma ufanisi wa kazi zao.

 Hata hivyo wamesema bado kama mamlaka wanafanya kazi katika mazingira magumu sana hasa pale wanapofanya upekuzi mizigo ya abiria hulazimika kutumia mikono na wala hawafahamu mizigo ile kama ipo salama ama laa. 

Wafanyakazi hao wamemuomba waziri huyo kufanya juhudi za makusudi kutafuta mashine alau moja ya kupimia mizigo ya abiria ili waweze kugundua ndani ya mizigo kuna kitu gani. 

Aidha wamemtaka waziri huyo kuchukua hatua maalumu kwa gari zinazoingia ndani ya kiwanja kwani wamesema kuna baadhi ya gari zinazokuja kuchukua viongozi huingia ndani ya uwanja jambo ambalo limekuwa likiharibu barabara za ndege yaani( apron). 

Kwa upande wake waziri Seif amesema lengo haswa la kufanya ziara katika taasisi mbali mbali za wizara yake ni kuangalia mapungufu yaliyopo ili kuhakikisha mapungufu hayo yanapatiwa ufumbuzi yakinifu. 

Aidha Waziri seif aliwatoa wasiwasi wafanyakazi hao kuwa hakuna tofauti katika ya kiwanja cha ndege unguja na cha pemba hivyo alimtaka meneja msaidizi kuhakikiksha kuwa hudma zinazotolewa unguja lazima Pemba ziwepo. 

Sambamba na hayo aliwataka wafanya kazi hao kubadilika katika utendaji wao na wawe wabunifu ili waweze kujitangaza ndani na nje ya nchi. Hata hivyo uwanja wa ndege ni sehemu nzito ya kufanya kazi ambapo alisema kila aliepewa dhamana ahakikishe anawajibika ipasavyo kwa vile kazi ni sehemu ya maisha yao. 

 Baada ya mazungumzo hayo mhe Waziri alitembelea jingo hilo kwa kukagua sehemu ya choo ambavyo vimefanyiwa matengenezo, sehemu ya zima moto na kuangalia mnara wa zantel ambao upo karibu na eneo la kiwanja hicho.

No comments: