Tuesday, September 27, 2016

TAMASHA LA UTAMADUNI HYDOM LATUMIKA KUFIKISHA UJUMBE WA UTUNZAJI WA MAZINGIRA MBULU


Kila mwaka shirika la Four Corner Culture Program (4CCP) huandaa tamasha la kiutamaduni ili kukuza na kuenzi tamaduni halisi za kitanzania . Tamasha la mwaka huu limekuwa lakipekee sana kutokana matukio mablimbali ya kimaendeleo na kiutamaduni yaliyofanyika .Ambapo Shirika la Norwegian Church Aid kwa kushirikiana na 4CCP Hydom walizindua miradi mbali mbali ya maendelea katika sekta ya maji (Visima)ili kupunguza tatizo kubwa la maji linalo wakumba wananchi wa wilayani Mbulu mkoani Manyara na mkoa jirani wa Singida.
Naibu Balozi Norway bwana TRYGVE BENDIKSBY .akizindua kisima cha maji kijiji cha ENDAGAW wilayani Mbulu. kutoka kulia ni TALE HUNGNES Mwakilishi Mkazi wa Shirika la NCA Tanzania,Mkuu wa wilaya ya Mbulu Mh.Flatey Massay, Balozi Msaidizi TRYGVE BENDIKSBY, Bwana Abeli Mfanyakizi wa NCA na Afisa Mradi wa WASH NCA Tanzania Bwana.Zakayo Makobelo.PICHA ZOTE NA IMANI NSAMILA.


Bwana Zakayo Makobelo akitoa ufafanuzi Juu ya kisima hiki kitumiacho Nishati ya Jua.

Mbunge wa Jimbo la Mkalama Mh.Allan Kilawa akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wa kijiji cha Munguli wilayani Mkalama Mkoani Singida.

Mkuu Wa wilaya ya Mkalama Mkoani Singida na Mbunge wa Mkalama wakionyweshwa Vifaa vifaa hivi vya kuzilisha nishati ya jua kwa ajili ya kusaidia Usamabazaji wa maji kijjijni.

Naibu Balozi wa Norway Tanzania TRYGVE BENDIKSBY alipotembelea banda la NCA NA 4CCP HYDOM wakati wa Tamasha la Utamaduni Hydom.

Vijana wa YouthCAN wakitoa elimu YA MAZINGIRA,AFYA NA MAJI SALAMA kupitia muziki wakati wa Tamasha la kiutamaduni.

No comments: