Thursday, February 5, 2015

DKT JOHN POMBE MAGUFULI AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA

 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mkandarasi pamoja na Mhandisi Mshauri wa barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya yenye jumla ya  km 89.3 inayojengwa kwa kiwango cha lami. Mradi huu utakapokamilika na kupokelewa na Serikali Mkandarasi atakaa site miaka mitatu kwa ajili ya uangalizi na kufanya marekebisho yoyote yatakayojitokeza kwa gharama zake mwenyewe.
 . Sehemu ya barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya yenye jumla ya  km 89.3 inayojengwa kwa kiwango cha lami. Barabara hii imekamilika kujengwa kwa asilimia 97.
 Sehemu unapojengwa mzani utakaotumika kupimia magari makubwa yatakayopita kwenye barabara hiyo.

 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Itigi waliofika kumpokea kabla ya kuwahutubia wananchi kuhusu maendeleo ya mradi huo wa barabara.
 Sehemu ya barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya (km 89.3) katika eneo la Itigi kama unavyoonekana.
 Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Patrick Mfugale akisoma taarifa ya ujenzi wa barabara Manyoni-Itigi-Chaya (km 89.3) inayotarajia kukamilika hivi karibuni.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika mkutano huo
 Waziri wa Ujenzi akiagana na baadhi ya  Wanafunzi wa shule ya Sekondari Itigi mara baada ya kuhutubia mkutano huo uliofanyika Itigi mkoani Singida.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe kushoto  akijadiliana jambo na Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Patrick Mfugale katikati kuhusu mradi wa ujenzi huo wa barabara
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli katikati akitoa maelezo kwa watendaji wa Wizara ya Ujenzi pamoja na TANROADS kabla ya kuanza kukagua barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya yenye jumla ya  kilometa 89.3.

No comments: